Wednesday, April 23, 2014

RAIS KIKWETE ATOA POLE KWA NDUGU KATIKA AJALI ILIYOTOKEA SIMIU

RAIS wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Ndugu Jakaya  Kikwete, amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Ndugu Pascal Mabiti, kuomboleza vifo vya watu 11 ambao wamepoteza maisha yao katika ajali ya basi iliyotokea jumatatu April 21,2014.

Aidha, katika salamu hizo raisi kikwete amesema kuwa ni jambo la kusikitisha kuwa ajali za barabarani zinaendelea kuchukua maisha ya watu wasiokuwa na hatia kila kukicha. Ameongeza, Naungana nao katika kuomboleza wapendwa wao. Napenda wajue kuwa msiba wao ni msiba wangu pia. Naungana nao katika kumwomba mwenyezi mungu mwingi wa rehemz aziweke peponi roho za marehemu.

Pia Rais Kikwete, ametoa pole kwa familia za wote waliopoteza ndugu, jamaa na marafiki katika ajali hiyo.

No comments:

Post a Comment