Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia, akiongea na wajumbe wa halimashauli kuu Taifa leo jijini Dar Es Salam. |
Baadhi ya Wajumbe wa halmashaul kuu Taifa wa NCCR Mageuzi, wakiwa wamesimama ili kuwakumbuka baadhi ya viongozi wa chama hicho waliotangulia mbele ya haki. |
MWENYEKITI wa Chama cha NCCR- Mageuzi, James Mbatia,
amewataka
wajumbe wa halmashauri kuu wa chama hicho, kudumisha misingi ya amani nchini ambayo hivi sasa imepotea.
wajumbe wa halmashauri kuu wa chama hicho, kudumisha misingi ya amani nchini ambayo hivi sasa imepotea.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, wakati wa kufungua
semina ya kujenga viongozi wa chama hicho, alisema kuwa amani ya nchi hii
imeanza kupotea kutokana na uongozi mbaya wa chama tawala ambacho kipo
madarakani.
“Tanzania ilikuwa ni kisima cha amani, lakini hivi sasa amani
imetowea kulingana na ubinafsi ambao ni chanzo kikubwa cha ufisadi, sisi hatuko
tayari kuona amani yetu ikipotea”alisema.
Aliongezea kuwa, sifa ya kuwa kiongozi bora ni kuonesha njia
sahihi, si kukaa kimya kuona mabaya yakitokea ndipo uanze kuchukua hatua.
Aliwataka viongozi wa chama hicho, kufata na kuiga misingi ya
amani ambayo baba wa Taifa Mwl Julius Nyerere aliiacha, jambo ambalo litakuwa
muhimili wa NCCR kwa kupata viongozi bora na wenye sifa ambayo watanzania wanahitaji.
Pia aliwapongeza wajumbe na wabunge wa chama hicho, kwa
kutohudhulia kwenye vikao vya Bunge Maalmu la Katiba, kwani kwa kufanya hivyo
inaonesha nidhamu ndani ya chama.
No comments:
Post a Comment