Tuesday, August 12, 2014

WEREMA NA SOFIA SIMBA NUSRA WADUNDANE KIKAONI

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba 
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba nusura wapigane baada ya kupishana kauli wakati wa mjadala wa ndani ya Kamati Namba Sita inayoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira.

Habari kutoka ndani ya kamati hiyo inayofanyia vikao vyake katika moja ya kumbi za Dodoma Hoteli zinasema, mvutano huo ulitokea Alhamisi iliyopita na kusababisha Wassira kusitisha kwa muda kikao hicho, kisha kwenda kuwasuluhisha.

No comments:

Post a Comment