![]() |
Mwenyekiti wa Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikil. |
Mwenyekiti wa Democratic Party (DP), Mchungaji
Christopher Mtikila amesema ameanza kukusanya saini za Watanzania
wanaopinga kuendelea kwa Bunge hilo ili kufungua kesi Mahakama Kuu ya
Tanzania, kusitisha vikao vinavyoendelea mjini Dodoma.
Mchungaji Mtikila akizungumza na Mwananchi
Jumapili alisema mchakato wa kukusanya saini hizo unaendelea katika
mikoa ya Arusha, Mwanza, Geita, Kagera, Dar es Salaam huku akibainisha
kwamba mwitio wa watu ni mzuri.
“Natafuta saini 20,000 za Watanzania na sasa
tayari tumekusanya saini zaidi ya 10,000 katika mikoa kadhaa na
natarajia Watanzania wataendelea kuniunga mkono ili kuhakikisha mchakato
huu. Nakwenda kuuzuia Mahakama Kuu na ninajua tu nitashinda,” alisema
Mchungaji Mtikila.
No comments:
Post a Comment