KOCHA WA SERENGETI BOYS ATAMBA KUITWANGA AFRIKA KUSINI CHAMAZI
Kikosi cha Serengeti Boys
Kocha Mkuu wa Serengeti Boys,
Hababuu Ali Omari amesema morali ya wachezaji wake ipo juu kwa ajili ya
mechi dhidi ya Afrika Kusini (Amajimbos) itakayochezwa kesho (Julai 18
mwaka huu).
Mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya
pili ya michuano ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17
itafanyika kwenye Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi jijini Dar es
Salaam kuanzia saa 10 jioni.
Akizungumza kwenye mkutano na
waandishi wa habari kwenye ofisi za TFF jijini Dar es Salaam leo, Kocha
Hababuu amesema nia ya kikosi chake ni kuhakikisha wanafika kwenye
fainali za Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Niger.
No comments:
Post a Comment