Saturday, July 19, 2014
FIFA YAONDOA ZUIO LILILOIWEKEA NIGERIA
Shirikisho la soka duniani FIFA limendoa marufuku lililoiwekea Nigeria.
Shirikisho hilo lilikuwa limeipiga marufuku Nigeria kutoshiriki katika michuano yoyote ya soka mapema mwezi huu kwa kuwa serikali ya Nigeria iliingilia uongozi wa shirikisho hilo nchini Nigeria.
Hatua hiyo ya kuondoa marufuku hiyo inajiri baada ya mahakama kuondoa agizo la kuwatoa baadhi ya maafisa wakuu wa shirikisho hilo nchini Nigeria.
Kwa miongo kadhaa serikali za afrika zimekuwa na ushawishi wa mashirikisho ya soka katika mataifa yao hadi FIFA ilipoondoa uwezo huo.
SOURCE BBC SWAHILI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment