Thursday, August 21, 2014

WALIOKUFA KWA EBOLA YAFIKIA 1,350


Mgonjwa wa Ebola akipelekwa eneo maalum kwa matibabu nchini Sierra Leone.
 
IDADI ya watu waliopoteza maisha kwa ugonjwa wa Ebola huko Afrika Magharibi mpaka sasa imefikia 1,350 kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Shirika la Afya Duniani (WHO) huku watu 106 wakiripotiwa kufariki kati ya Agosti 17-18 mwaka huu.
Ugonjwa huo ambao husambazwa moja kwa moja kupitia majimaji ya mwilini kutoka kwa mgonjwa mpaka sasa bado hauna tiba.

No comments:

Post a Comment