Monday, July 21, 2014

KESI ZA MAHABUSU WALIOVUA NGUO GEITA ZAANZA KUSIKILIZWA

IKIWA takribani  mwezi mmoja baada ya Mahabusu wanane wa gereza la wilaya ya  Geita mkoani Geita kuvua nguo na kubaki utupu katika mahakama ya Mwanzo ya Nyankumbu kwa madai ya kucheleweshwa kesi zao huku wakitaka mamlaka husika ikiwa mwanasheria wa serikali ,jaji na mkuu wa mkoa wawasikilize madai yao hatimaye kesi zao zimeanza kusikilizwa jana katika mahakama ya wilaya.

Mbele ya Hakimu wa mahakama ya wilaya Kario Mrisho ,wakili wa serikali Erasto Anosisye alidai kuwa kati ya mahabusu wanana,wanne wana kesi ya mada na wanne wana kesi ya kuvunja na kuiba ambayo imeanza kusikilizwa huku wa kesi ya mada inasubiri mahakama kuu kwa vile mahakama ya wilaya haina uwezo wa kusikiliza kesi hizo.

Katika mashitaka ya kuvunja na kuiba   inadaiwa kuwa washitakiwa ambao ni Iriza Warioba(26) mkazi wa katundu,Joseph Mrefu(28) mkazi wa Runzewe,Silvester Emmanuel(22) mkazi wa katundu na Saimon Panya(22) mkazi wa msufini mjini Geita mnamo tarehe 3 mwezi 11 2013 majira ya saa tatu usiku katika kijiji cha Nyamulilima kata ya Mtakuja wilayani Geita watuhumiwa walivunja na kuiba solar power 2,Betry 5,tv,na vifaa vingine kwenye kampuni la ujenzi ya Hircon Construction Compay inayofanya kazi katika mgodi wa Geita Gold Mine vyenye thamani ya shilingi 19,530,000/=na kutokomea kusikojulikana.

Aidha mara baada ya kukimbia kusikojulikana mlinzi aliyekuwepo siku hiyo alienda kutoa taarifa na baada ya mda mfupi walifuatiliwa na kukamatwa na kufikishwa katika kituo cha polisi cha Mgusu kabla hawajapelekwa mahakamani.

Baada ya kusomewa mashitka yao watuhumiwa wote wanne walikana kosa hilo na hakimu Mrisho aliahirisha kesi hiyo hadi tarehe 31 mwezi huu huku watuhumiwa wakirudishwa rumande baada ya kukoswa vigezo vya dhamana.

Watuhumiwa hao mwezi uliopita walileta tafrani baada ya kunga'anga'nia mlingoti wa bendera huku wakiwa uchi  walipokuwa wameletwa mahakamani kusikilizwa kesi zao  wakidai kuwa wamekuwa wanakuja mahakamani bila ya kusikilizwa kesi zao hivyo hawajui hatma yao na kumtaka mkuu wa mkoa na viongozi wengine wanaohusika wawasikilize.

 Hata hivyo katibu tawala wa wilaya alifanikiwa kuwaelewesha na kutoka hapo kwa ahadi ya kutatua kero zao ambapo siku hiyo jopo la mahakimu wa wilaya na mahakama ya mwanzo,mwanasheria wa serikali pamoja na ofisi ya upelelezi mkoa walienda katika gereza hilo mnamo saa 8 na kusikiliza kero zao wote na ambao hawakugoma wakiwemo wafungwa na mahabusu.

Na Valence Robert-Malunde1 blog-Geita

No comments:

Post a Comment