Tuesday, August 5, 2014

RAGE APATA AJALI YA GARI



MWENYEKITI wa Simba aliyemaliza muda wake, Ismail Aden Rage, jana amenusurika kifo baada ya kupata ajali ya agari eneo Chigongwe, nje kidogo ya Manispaa ya Dodoma, wakati akiingia mjini humo kwa ajili ya kuhudhuria vikao vya Bunge Maalum la Katiba linaloanza leo.

Kwa mujibu wa taarifa zilizolifikia Mtandao huu wakati likienda mitamboni, zilisema kuwa Rage amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Dodoma, akiwa na majeraha aliyoyapata yeye na watu wengine alioongozana nao katika gari moja.

No comments:

Post a Comment