Monday, July 28, 2014
MAKANISA YANAYOENDEKEZA VURUGU KUFUTILIWA MBALI
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe amesema yeye mwenyewe atayafuta makanisa yote yanayoleta vurugu na uvunjifu wa amani kwa kuwa hayatoi taswira ya kile wanachopaswa kufanya na ni aibu kwa Mungu wanayemtumikia.
Amesema ni aibu kwa viongozi wa makanisa kupigana hadharani wakati wa Ibada na kupishana katika vituo vya Polisi wakishtakiana jambo alilosema linachochea shari na kuharibu nchi.
Amelitaja kanisa mojawapo ambalo lina vurugu kuwa ni Kanisa la Moravian, Jimbo la Misheni Mashariki ambalo kwa zaidi ya miaka miwili sasa sharika zake zimekuwa na vurugu inayohusisha uongozi na ubadhirifu wa mali.
"Serikali haitavumilia vitendo vya vurugu katika makanisa na ikibidi mimi mwenyewe nitayafuta usajili wa hayo makanisa yenye migogoro kuepusha shari," alisema Chikawe jana katika ibada maalumu ya kuombea Taifa amani, utulivu na uzalendo wa kweli.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment