Mjumbe
wa Kamati ya utendaji MISA -TAN, Lilian Lucas Kasenene akimpongeza
Mwenyekiti mpya wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika, Tawi
la Tanzania (MISA-TAN), Simon Berege.
Na Nathaniel Limu
Mkutano
mkuu wa uchaguzi wa Chama cha waandishi wa habari kusini mwa Afrika
(MISA-TANZANIA), umemchagua kwa kishindo Mhadhiri wa Chuo kikuu cha
Iringa, Simon Berege kuwa mwenyekiti wake kwa kipindi cha miaka mitatu
ijayo.Berege ambaye alikuwa mgombea pekee wa nafasi hiyo, alizoa kura zote 26 za ndio zilizopigwa.Ushindi
huo ni wa asilimia mia moja wa kura zote zilizopigwa na wajumbe wa
mkutano huo uliofanyika kwenye ukumbi wa makao makuu ya MISA-TAN uliopo
Mkwajuni Mwananyamala jijini Dar-es-salaam.
Mhadhiri
huyo ambaye pia ana taaluma ya uandishi wa habari,amechukua nafasi hiyo
iliyokuwa inashikiliwa na Mwanasheria Mohammed Tibanyendera,
aliyemaliza muda wake.
Mwenyekiti
wa mkutano huo wa uchaguzi,Tibanyendera,aliwatangaza Liliani Lucas
Kasenene na Abdala Mohammed Mmanga kuwa wajumbe wa kamati ya utendaji,
baada ya kupata kura 23 (za Liliani) na 17 (za Mmanga).Mgombea mwingine
wa nafasi hiyo,Timoth Kitundu,aliambulia kura nane.
Tibanyendera
alisema nafasi za makamu mwenyekiti na ile ya mweka hazina,zitatangazwa
baadaye kutokana na kukosekana na wagombea katika nafasi hizo, licha ya
kutangazwa sana.
Akiwashukuru
wapiga kura wake, Mwenyekiti mteule Barege, alisema ushindi wa asilimia
mia moja ,hauwezi kusababisha yeye abweteke na badala yake utakuwa
chachu kwake ya kuchapa kazi kwa bidii na maarifa ili kukidhi matarajio
ya wapiga kura wake.
Katika
hatua nyingine ,taarifa ya fedha ya MISA-TAN kwa mwaka jana,
imebainisha kuwa taasisi hiyo inadaiwa zaidi ya shilingi 124.3 milioni
na wadau mbalimbali.
Ilidaiwa
kwamba mamlaka ya mapato Tanzania (TRA),inadai zaidi ya shilingi 93.1
milioni, mkaguzi wa mahesabu 1.6 milioni na mfuko wa NSSF,2.9 milioni.
Kwa
mujibu wa taarifa hiyo,taasisi hiyo imekusanya mapato ya zaidi ya
shilingi 141.2 milioni kutoka kwenye vyanzo vyake mbalimbali vya mapato
kwa kipindi cha mwaka jana,kati ya matarajio ya kukusanya zaidi ya
shilingi 322.9 milioni iliyotatajia kukusanya.
No comments:
Post a Comment