Tuesday, August 5, 2014

KIKWETE AJIBU TUHUMA ZA RIDHIWANI NA UNGA


RAIS Jakaya Kikwete amesema ni mkusanyiko wa upuuzi kudai kuwa alishiriki kumwokoa mtoto wake, Ridhiwani, aliyedaiwa kukamatwa na dawa za kulevya nje ya nchi.

Alisema urais ni taasisi kubwa nchini na hivyo hawezi kujiingiza katika ubishani na watu wa mtaani, kama ambavyo baadhi yao wanamsukuma ashiriki katika maneno hayo ya mitaani.

“This is nonsense (huu ni ujinga), na ni mkusanyiko wa upuuzi, sina muda wala siwezi kupoteza nguvu yangu kujadili upuuzi na ujinga wa namna hiyo,” alisema Kikwete wakati alipokuwa akizungumza na Watanzania waishio Marekani alipokutana nao Agosti 2, mwaka huu mjini Washington D.C.

Rais Kikwete ambaye yuko katika ziara ya kikazi ya siku tisa nchini Marekani, alisema hayo wakati akijibu maswali kuhusu madai yaliyotolewa Julai Mosi mwaka juzi, na Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa.

“Hatuwezi sisi kujiingiza katika shughuli ya kupoteza muda kwa kushiriki upuuzi na ujinga. Haya ni maneno ya kipuuzi yanayosemwa na watu ambao kazi yao usiku na mchana ni kuota jinsi ya kuyumbisha ajenda yetu ambayo imefanikiwa sana katika kubadilisha hali ya maisha ya Watanzania,” aliongeza.

No comments:

Post a Comment