Tuesday, April 22, 2014

TASISI ZA KIISLAM NCHINI ZAMSHUKIA WAZIRI LUKUVI.


Waziri wan chi Ofisi ya Waziri mkuu Willium Lukuvi (picha kutoka maktaba)




TAASISI za kiislam Tanzania, zimepokea kwa masikitiko kauli za kichochezi zinazotolewa na baadhi ya viongozi wa juu serikalini.

Akiongea na waandishi wa habari mda mfupi uliopita hivi leo, msemaji wa Tasisi hiyo Rajabu Katimba  amesema kuwa Waziri wan chi Ofisi ya Waziri mkuu Willium Lukuvi juzi ametoa kauli za kichochezi katika kanisa la Mchungaji Joseph huko Dodoma.


“Mh Lukuvi alitamuka wazi kwamba serikali tatu zikipita eti nchi nchi itakosa Amani! Alikwenda mbali na kutamka kuwa wanaotaka nchi yao ni WAZANZIBARI hawawezi kujitegemea bali wanataka serikali ili wapate nafasi ya kujitangaza kuwa nchi ya kiislamu,”alisema.

Aliongezea kuwa, kauli hizo za kichochezi zinathibidisha kile ambacho waislam wanakilalamikia kwa mda mrefu sasa, juu ya kuwepo kwa mfumo wa kristo unaotawala nyuma ya pazia.
Rajabu alisema kuwa, kwa miaka zaidi ya 40 sasa waislamu wanalalamikia juu ya kuwepo na mfumo wa Kikristo unaojali maslahi ya dini moja, ubaguzi huu ambao wamenza kuonesha utapeleka nchi hii sehemu mbaya.

Alihoji kuwa, je kauli kama hizi zinatolewa na viongozi wa serikali, mwislamu kushutumu ukristo ndani ya msikiti hali ingekuwaje kwa kiongozi huyo?

Hatahivyo alisema kuwa, hadi hivi sasa hakuna hatua zozote za maana zilizochukuliwa na mamlaka husika dhidi ya kiongozi huyo kwa kauli zake za Kibaguzi, mchozi na mwenye chuki  za wazi dhidi ya watanzania wapenda Amani na waislamu kwa ujumla.

Taasisi hiyo, imeadhimia kuwa Mh Lukuvi ajiuzuru au Rais amwajibishe, serikali ikanushe kwa uwazi na kuomba radhi kwa waislamu na watanzania kwa ujumla, rasimu ya katiba iliyowasilishwa katika bunge la katiba iheshimiwe kwa mujibu wa sharia ya mabadiliko, maoni ya makundi mbalimbali yaheshimiwe.

Pia aliwataka Waislamu na wakristo na wananchi wote kwa ujumla kuendeleza mshikamano wao katika kutengeneza katiba mpya yenye maridhiano yatakayoondoa kero za watanzania.

1 comment: